Ukiongeza saa nyingine 7 za kulala, inamaanisha unatumia robo tu ya muda wako ukiwa umesimama au ukiwa unatembea kwa siku ambapo muda huo mfupi wa kutuliza mwili unazidisha hatari ya unene lakini pia orodha ya maradhi mengine kama matatizo ya moyo, kisukari, saratani, magonjwa ya misuli, mgongo, mshtuko n.k
Shirika la afya duniani limegundua kwamba kukaa bila kufanya kitu chochote ni chanzo cha nne kinachoua watu kwa kasi zaidi duniani ambapo pia ukiachana na kuongeza unene katika mwili imekua ikigharimu uchumi wa nchi ya Uingereza bilioni 145 kila mwaka kutokana na matatizo ya mgongo na misuli.
Shirika la afya duniani linashauri angalau kwa wiki mtu afanye mazoezi kwa dakika 150 ambazo ni sawa na saa mbili na dakika 40 ambapo ushauri mwingine ni wa labda dakika 30 kwenye siku tano, hiyo ni angalau kuliko kutumia muda mwingi kuketi ambako ni hatari kwa afya.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni